Jumanne, 31 Desemba 2024

TANGA, KITUO CHA UTALII WA KIHISTORIA NA KIUTAMADUNI CHENYE MCHANGO MKUBWA KWA UCHUMI NCHINI TANZANIA.

Mkoa wa Tanga ni eneo lenye historia na utajiri wa kitamaduni, likiwa na vivutio vya kipekee vinavyovutia watalii wa ndani na nje ya nchi. Baadhi ya vivutio maarufu vya utalii mkoani Tanga ni Mapango ya Amboni, ambayo ni mapango makubwa zaidi Afrika Mashariki, na mji wa kihistoria wa Pangani wenye urithi wa kihistoria wa biashara ya utumwa na harakati za uhuru. 

 

Pia, Hifadhi ya Taifa ya Saadani ni kivutio adimu kinachochanganya mandhari ya wanyamapori na fukwe za bahari, huku Visiwa vya Maziwe vikivutia kwa shughuli za kuogelea, kupiga mbizi, na uchunguzi wa viumbe wa baharini. Aidha, Urithi wa Mji Mkongwe wa Tanga unabeba thamani ya kihistoria inayovutia watafiti na wageni.  

 

Kwa mujibu wa takwimu za mwaka 2023, Tanga ilipokea jumla ya watalii 150,000, ambapo 30% walikuwa wageni kutoka mataifa mbalimbali. Sekta ya utalii ilichangia takriban TZS bilioni 25 katika uchumi wa mkoa, huku ikitoa ajira zaidi ya 10,000 kwa wakazi wa eneo hilo moja kwa moja.  

 

Vivutio hivi vinaendelea kushikilia nafasi muhimu katika kukuza utalii endelevu, huku serikali na wadau wakihamasisha uwekezaji zaidi ili kuboresha miundombinu na huduma za utalii mkoani Tanga. 

Ijumaa, 27 Desemba 2024

UKUAJI WA UCHUMI WA TANZANIA, TAKWIMU NA MAFANIKIO YA MIAKA MITATU (2021-2023)

Tanzania imekuwa ikishuhudia ukuaji thabiti wa uchumi kwa miaka kadhaa. Kwa mujibu wa Benki ya Dunia na Taasisi ya Takwimu ya Taifa (NBS), ukuaji wa uchumi wa Tanzania ulikuwa kama ifuatavyo:  

 

2021, Uchumi ulikua kwa asilimia 4.9, licha ya changamoto za janga la COVID-19. 

 

2022, Ukuaji uliongezeka hadi asilimia 5.3, ukichochewa na miradi mikubwa ya maendeleo kama SGR, Mwalimu Nyerere Hydropower, na EACOP.  


2023, Uchumi ulionyesha kasi zaidi kwa ukuaji wa asilimia 5.8, ukihamasishwa na ongezeko la uwekezaji wa ndani na nje.  

 

Sekta zilizoongoza katika ukuaji wa uchumi ni pamoja na.. 

Kilimo: Huchangia takriban asilimia 26.9  ya Pato la Taifa (GDP).  

 

Ujenz: Ulichangia kwa asilimia 14.3 kutokana na miradi mikubwa ya miundombinu. 

 

Utalii: Mapato ya utalii yalifikia Dola za Marekani 2.6 bilioni mwaka 2023, yakirejea kutoka athari za COVID-19.  

 

Ukuaji huu umeimarisha maisha ya Watanzania, kupunguza umaskini, na kuimarisha huduma za msingi kama elimu, afya, na maji safi.

JE, WAJUA! UMOJA WA WATANZANIA NI MFANO WA KUIGWA NA SIO NDOTO TENA?

Tanzania imeendelea kuwa mfano wa kuigwa barani Afrika na duniani kwa kusimamia misingi ya umoja, mshikamano, na utawala wa sheria. Umoja wa kitaifa umebaki kuwa nguzo muhimu katika kuimarisha amani, utulivu, na maendeleo ya nchi, huku ukijengwa juu ya msingi madhubuti wa katiba na sheria za nchi.  

Sheria za Tanzania zimetungwa kwa kuzingatia misingi ya usawa, haki, na kuheshimu utu wa binadamu. Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 imeweka bayana kwamba nchi hii ni moja, yenye watu wa makabila, dini, na tamaduni mbalimbali. Hii imekuwa dira ya kuimarisha mshikamano kwa kuhakikisha kwamba kila Mtanzania anahisi kuwa sehemu ya taifa bila kujali tofauti zao za kijamii au kiitikadi.  

 

Sheria zinazozuia ubaguzi wa aina yoyote zimeimarisha umoja wa kitaifa. Mathalani, Sheria ya Makosa ya Jinai (Penal Code) inahakikisha kwamba vitendo vyote vya uchochezi wa kikabila, kidini, au kijamii vinakabiliwa kwa mujibu wa sheria. Hali hii imewezesha Tanzania kudumu katika hali ya amani na utulivu kwa zaidi ya nusu karne tangu uhuru.  

 

Taratibu za kitanzania, kama vile kuheshimu mamlaka za kijamii, kushiriki katika maadhimisho ya kitaifa, na kuzingatia mila na desturi za Watanzania, zimekuwa sehemu muhimu ya kudumisha mshikamano. Maadhimisho kama Siku ya Uhuru, Muungano, na Mashujaa huwakutanisha Watanzania kutoka pande zote za nchi kusherehekea na kuthamini historia ya pamoja.  

 

Aidha, Tanzania imejikita katika sera zinazolenga kuimarisha umoja, kama vile Sera ya Elimu ya mwaka 2014 inayosisitiza matumizi ya Kiswahili kama lugha ya kufundishia, ambayo imeendelea kuwa kiunganishi kikuu kwa Watanzania wote.  

Umoja huu ni matokeo ya juhudi za pamoja za wananchi na viongozi waliochaguliwa kwa misingi ya demokrasia.  

 

Kwa sasa, Tanzania inajivunia kuwa na mazingira salama ya kibiashara, maendeleo ya miundombinu, na huduma za kijamii ambazo zinawanufaisha watu wa makundi yote. Mfano hai ni utekelezaji wa miradi mikubwa ya kitaifa, kama vile reli ya kisasa (SGR), mradi wa Bwawa la Mwalimu Nyerere, na miradi ya maji inayohakikisha Watanzania wanapata huduma muhimu bila ubaguzi.  

 

Ili kuhakikisha kwamba umoja wa Tanzania unadumu kwa vizazi vijavyo, ni muhimu kuendelea kutoa elimu ya uraia, kusimamia haki za binadamu, na kuhakikisha kila mtu anashiriki kikamilifu katika maendeleo ya nchi. Viongozi wa kisiasa, kijamii, na kidini wanapaswa kuendelea kuwa mfano bora wa mshikamano, huku wakiwaelimisha wananchi kuhusu umuhimu wa kuheshimu sheria na taratibu za nchi.  

 

Kwa hakika, umoja wa Tanzania sio ndoto tena, bali ni ukweli unaoishi ndani ya mioyo ya Watanzania. Kwa kushikamana na misingi ya sheria na taratibu, taifa hili linaendelea kuwa kisiwa cha amani na mshikamano katika bara la Afrika.  

 

#SioNdotoTena  

Jumanne, 24 Desemba 2024

JE, MRADI WA MABASI YA MWENDO KASI (BRT) JIJINI DAR ES SALAAM NI SULUHISHO LA KUDUMU KWA CHANGAMOTO ZA USAFIRI?

Mradi wa Mabasi ya Mwendo Kasi (BRT) jijini Dar es Salaam ni mojawapo ya miradi muhimu zaidi ya miundombinu nchini Tanzania, ukilenga kuboresha usafiri wa umma na kupunguza changamoto za msongamano wa magari. Tangu kuanzishwa kwake, mradi huu umeleta mabadiliko makubwa kwa wakazi wa jiji hilo.

Awamu ya kwanza ya BRT ilianza kazi rasmi mwaka 2016, ikiwa na kilomita 21.1 za barabara maalum za mwendo kasi, vituo 27 vya kisasa vya mabasi, na daraja kubwa la Tazara. Awamu hii ilihudumia takribani abiria 200,000 kila siku, ikisaidia kupunguza muda wa safari na gharama za usafiri kwa wakazi wa Dar es Salaam. 

 

Utekelezaji wa awamu nyingine za mradi unaendelea kwa kasi. Awamu ya pili, yenye kilomita 20.3 kutoka Mbagala hadi katikati ya jiji, imekamilika kwa asilimia 95, huku gharama za mradi huu zikifikia zaidi ya shilingi bilioni 290. Mabasi yameanza majaribio, na matarajio ni kuanza huduma rasmi hivi karibuni. Awamu hii inatarajiwa kuhudumia wakazi wa maeneo ya kusini mwa jiji, ambayo awali yalikuwa na changamoto kubwa ya usafiri.

 

Awamu ya tatu ya mradi, inayohusisha kilomita 23.6 kutoka Gongo la Mboto hadi Kariakoo kupitia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), imekamilika kwa asilimia 70. Barabara hii itaunganisha maeneo muhimu ya biashara na uchumi, na pia kuboresha usafirishaji wa abiria na mizigo ndani ya jiji.

 

Kwa ujumla, mpango wa BRT unalenga kujenga zaidi ya kilomita 130 za barabara maalum za mwendo kasi. Hadi sasa, zaidi ya kilomita 64 zimekamilika na ziko katika matumizi. Mradi huu unatarajiwa kupunguza muda wa safari kwa wastani wa asilimia 50, kupunguza uchafuzi wa mazingira kwa kutumia mabasi yanayotumia nishati safi, na kuboresha hali ya hewa ya jiji. Pia, unatoa ajira kwa maelfu ya vijana, ikiwa ni pamoja na madereva, wahudumu wa vituo, na mafundi wa matengenezo ya miundombinu.

 

Faida za mradi huu kwa Watanzania ni nyingi. Kwanza, umeongeza ufanisi wa usafiri wa umma kwa kuwapa wananchi chaguo la usafiri wa haraka na salama. Pili, mradi huu umechangia katika kukuza uchumi wa maeneo ya jirani, kwani watu wengi sasa wanaweza kufikia maeneo ya kazi na biashara kwa urahisi. Tatu, umeimarisha hadhi ya Dar es Salaam kama jiji linaloendelea kwa kasi barani Afrika.

Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, akizungumza hivi karibuni, alisema: "Mradi wa Mabasi ya Mwendo Kasi ni zaidi ya mradi wa miundombinu. Ni mabadiliko ya kimkakati yanayolenga kuboresha maisha ya kila Mtanzania."

 

Kwa wakazi wa Dar es Salaam, mradi wa BRT ni kielelezo cha maendeleo na matumaini. Kadri awamu mpya za mradi zinapokamilika, BRT itaendelea kuwa nguzo muhimu ya usafiri wa umma nchini Tanzania na mfano wa mafanikio ya kisasa katika sekta ya miundombinu.

 

Alhamisi, 12 Desemba 2024

OFISI YA MKUU WA WILAYA NJENDENGWA, DODOMA: ALAMA YA MAENDELEO CHINI YA UONGOZI WA MHE. DKT. SAMIA SULUHU HASSAN

Dodoma, Tanzania - Ofisi ya Mkuu wa Wilaya iliyopo Njendengwa, ndani ya Jiji la Dodoma, ni mojawapo ya miradi muhimu ya ujenzi iliyotekelezwa katika awamu ya sita ya uongozi chini ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan. 

Jengo hili limejengwa kwa kuzingatia viwango vya kisasa, likiwa na miundombinu ya kisasa inayolenga kuboresha utoaji wa huduma za utawala na maendeleo kwa wananchi wa Wilaya hiyo. Kukamilika kwa jengo hili ni sehemu ya jitihada za serikali kuhakikisha miundombinu ya kisiasa na kiutawala inaimarishwa, ikiwa ni ishara ya dhamira ya Rais Samia katika kuleta maendeleo yenye tija kwa Taifa.  

Aidha, ujenzi wa ofisi hii ni sehemu ya mpango mpana wa serikali ya awamu ya sita wa kuboresha huduma kwa wananchi kwa kuhakikisha watendaji wa serikali wanakuwa na mazingira bora ya kufanyia kazi, hatua inayochangia ufanisi wa utoaji huduma na maendeleo katika ngazi za wilaya na mikoa.  

Wananchi wa Dodoma wamesifu juhudi za serikali kwa kuona kuwa Wilaya ya Dodoma imepewa kipaumbele, huku wakibainisha kuwa jengo hili litachochea maendeleo ya kiutawala na kijamii katika eneo hilo.  

KIWANDA CHA KUTENGENEZA NDEGE MOROGORO: MAENDELEO MAKUBWA YA AIRPLANE AFRICA LIMITED

 

Kampuni ya Airplane Africa Limited (AAL), inayomilikiwa na wawekezaji kutoka Jamhuri ya Czech, ilianzisha kiwanda cha kuunganisha na kutengeneza ndege mwaka 2021 katika eneo la Mazimbu, mkoani Morogoro. Kiwanda hiki ni cha kwanza barani Afrika katika sekta hii. 

Hadi kufikia Desemba 2024, AAL imefanikiwa kuunganisha na kutengeneza zaidi ya ndege tatu aina ya Skyleader 600, zenye uwezo wa kubeba abiria wawili hadi wanne. Ndege hizi zimeanza safari rasmi ndani na nje ya nchi, baada ya kupata cheti cha kuipasisha kutoka Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) mnamo Septemba 2024. 


Kiwanda hiki kimeajiri mafundi wengi ambao ni wahitimu wa Chuo cha Usafirishaji (NIT), hivyo kuchangia katika kutoa uzoefu kwa wanafunzi kutoka vyuo vikuu, vyuo vya kati, na vyuo vya ufundi. 

 

Serikali ya Tanzania, kupitia Wizara ya Uchukuzi, imeonyesha nia ya kusaidia sekta ya anga kwa kushirikiana na Wizara ya Fedha ili kuweka mazingira mazuri kwa wawekezaji kama AAL. Hatua hii inalenga kuimarisha uwekezaji na kukuza teknolojia ya utengenezaji wa ndege nchini. 

 

Kwa sasa, ndege zinazotengenezwa na AAL zinaweza kuuzwa katika nchi mbalimbali, na mipango ya baadaye ni kuunda ndege zenye uwezo wa kubeba abiria zaidi ya wawili. 

 

Kwa maelezo zaidi kuhusu kiwanda hiki na shughuli zake, unaweza kutembelea tovuti rasmi ya Airplane Africa Limited. 

 

 

KAMATI ZA ULINZI NA USALAMA, WATENDAJI WA MIKOA NA HALMASHAURI ZA MKOA WA MARA WAPIGWA MSASA JUU YA UTAWALA BORA NA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA


Wizara ya Katiba na  sheria imeanza kutoa  mafunzo ya utawala Bora  na Uraia kwa kamati za Usalama za Mikoa na Wilaya,wakuu wa idara mbalimbali za Halmashauri na watendaji wa Kata wilayani Rorya Mkoani Mara ili kuwakumbusha kuzingatia Mipaka katika utumishi wa umma na Misingi ya Utawala bora.

 


Akizungumza Wakati wa mafunzo hayo Wilayani Rorya Mkoani mara  Joyce mushi wakili wa serikali Mkuu kutoka Wizara ya Katiba na Sheria ambaye pia nimratibu wa mafunzo wa Elimu ya utawala Bora ambapo amesema Mafunzo hayo nimwendelezo wa mafunzo ambapo yalianzia Mkoa wa Rukwa huku walengwa wakuu wakiwa nikamati za Usalama watendaji wa kata na watumishi wa idara mbalimbali za Halmashauri.

 

Joyce alisema lengo la Mafunzo hayo nikuwakumbusha na kuwajengea uwezo washiriki ili waweze kuwa na Uelewa wakutekeleza majukumu Yao kwa kufata misingi ya utawala bora na haki za binadamu na demokrasia.

 


"Mafunzo hayo kutolewa niutekelezaji wa Falsafa ya Rais DKT Samia Suluhu Hassan ya 4R- ya Ujenzi upya(Rebuilding) ambapo tunaamini tukimaliza Mafunzo haya washiriki wote watakuwa wamejengwa upya na Kutekeleza majukumu yao kwa ufasaha kwa Wananchi"Joyce mushi wakili wa serikali Mkuu kutoka Wizara ya Katiba na Sheria"

 

Robhi Richard wambura Afisa mtendaji kata ya Roche nimiongoni mwa wanaufaika wa mafunzo hayo ambapo amemshukuru Rais DKT Samia Suluhu Hassan kupitia wizara ya Katiba na Sheria alisema mafunzo hayo yatasaidia kuwa chachu ya mabadiliko katika vituo vya kazi kutokana na kipindi cha Nyuma wengi wao walikuwa wanafanya kazi bila kuzingatia miiko na Mipaka yao yakazi.

 


Elimu ya Utawala bora na uraia kwa viongozi wa mamlaka za Serikali za mitaaa inaendelea katika Mkoa wa mara huku ikitarajiwa kufanyika katika Halmashauri zote za Mkoa huo wa Mara 

MAFUNZO YA URAIA NA UTAWALA BORA YAIMARISHA UWEZO WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA KATIKA MIKOA YA IRINGA NA MARA

Katika juhudi za kuimarisha utawala bora na kukuza uelewa wa masuala ya uraia, Wizara ya Katiba na Sheria imeendesha mafunzo kwa viongozi wa serikali za mitaa katika Halmashauri mbalimbali. Mafunzo haya ni sehemu ya utekelezaji wa falsafa ya 4R ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, yenye lengo la kujenga upya misingi ya utawala bora kwa viongozi wa ngazi za mitaa.



Katika mkoa wa Iringa, mafunzo yalifanyika kwa:  

1. ⁠Manispaa ya Iringa  

2. ⁠Halmashauri ya Wilaya ya Iringa  

3. ⁠Halmashauri ya Wilaya ya Kilolo  

 

Jumla ya washiriki 110 walihudhuria mafunzo haya, wakiwemo Kamati za Usalama za Wilaya, Wakuu wa Idara wa Halmashauri, na Watendaji wa Kata. Mada zilizojadiliwa ni pamoja na 

- Uraia na Utawala Bora  

Lengo kuu lilikuwa kujenga uwezo wa viongozi katika kutekeleza majukumu yao kwa weledi na kufuata misingi ya demokrasia.

 

Halmashauri ya Wilaya ya Rorya nayo ilijumuisha washiriki 38 waliogawanyika kama ifuatavyo 

- Watendaji wa Kata 26  

- Kamati ya Usalama ya Wilaya 5  

- Wataalamu wa Halmashauri 7  

 

MADA ZILIZOJADILIWA 

1. Haki na Wajibu  

2. Demokrasia na Utawala Bora  

3. Haki za Binadamu  

4. Madaraka ya Umma  

 


Mafunzo haya yalifunguliwa rasmi na Wakili wa Serikali Mkuu, Bi. Joyce Mushi, ambaye pia ni Mratibu wa Mafunzo haya.

 

Mafunzo haya yamelenga kuwajengea uwezo viongozi wa serikali za mitaa, hususan Kamati za Usalama, ili waweze kutekeleza majukumu yao kwa weledi, ufanisi, na kujiamini huku wakizingatia misingi ya haki za binadamu na utawala bora. Kupitia mafunzo haya, viongozi wanatarajiwa kupata ujuzi wa kuimarisha utoaji wa huduma kwa wananchi na kujenga jamii inayozingatia demokrasia na uwajibikaji.

 

Mafunzo haya yameanza katika mikoa ya Rukwa na sasa yanaendelea katika mikoa ya Mara, Morogoro, Iringa, na Songwe. Yanalenga kuhakikisha viongozi wanapokea mafunzo ya kina yatakayowasaidia kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi zaidi.

Mafunzo haya ni kiini cha utekelezaji wa falsafa ya "Rebuild" ya Rais Samia Suluhu Hassan, ikilenga si tu kuboresha utendaji kazi wa viongozi wa serikali za mitaa, bali pia kuwajengea uelewa wa umuhimu wa kuhudumia wananchi kwa weledi na kwa kuzingatia haki na demokrasia.   

Jumatano, 11 Desemba 2024

MAENDELEO YA MJI WA MTUMBA DODOMA, KITUO KIKUU CHA OFISI ZA SERIKALI TANZANIA

Mji wa Mtumba, uliopo jijini Dodoma, ni eneo maalum lililotengwa kwa ajili ya ofisi za Serikali ya Tanzania. Mpango wa kuhamishia makao makuu ya Serikali Dodoma ulianza rasmi mwaka 2016, na tangu wakati huo, maendeleo makubwa yamefanyika katika ujenzi wa mji huu.

Kufikia Mei 2024, jumla ya watumishi wa umma 25,039 na taasisi 65 tayari walikuwa wamehamia Dodoma na kuanza shughuli zao katika mji wa Mtumba.  Ujenzi wa awamu ya pili wa majengo ya ofisi za wizara na taasisi mbalimbali unaendelea, ambapo unatarajiwa kukamilika mwaka 2025.

 

Mnamo Julai 3, 2023, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alikagua maendeleo ya ujenzi wa mji wa Serikali Mtumba na kutoa maagizo kwamba ifikapo Oktoba mwaka huo, majengo yawe yamekamilika na kuwekwa samani, ili watumishi waanze kuyatumia ifikapo Januari 1, 2024. 


Mradi wa ujenzi wa mji wa Serikali Mtumba umeleta manufaa makubwa, ikiwa ni pamoja na kutoa ajira kwa wananchi na kuchochea ukuaji wa uchumi katika jiji la Dodoma.  Aidha, Serikali imekuwa ikisisitiza matumizi ya bidhaa zinazozalishwa nchini katika ujenzi huo, ili kuunga mkono viwanda vya ndani.

 

Maendeleo ya ujenzi wa mji wa Mtumba yamekuwa yakiridhisha, na Serikali inaendelea na jitihada za kukamilisha miradi iliyobaki kwa wakati ili kuhakikisha watumishi wa umma wanapata mazingira bora ya kufanyia kazi.


 MAFUNZO YA WAJUMBE WA KAMATI YA USALAMA KUHUSU ELIMU YA URAIA NA UTAWALA BORA  YANAYORATIBIWA NA WIZARA YA SHERIA NA KATIBA YANAFANYIKA MKOANI IRINGA



Iringa, Desemba 11, 2024  

Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Herry James, ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Iringa, amefungua rasmi mafunzo maalum ya kuwajengea uwezo wajumbe wa Kamati za Usalama za Mkoa wa Iringa. Mafunzo haya, yanayoratibiwa na Wizara ya Katiba na Sheria kwa kushirikiana na taasisi mbalimbali, yanafanyika kuanzia tarehe 11 hadi 13 Desemba 2024.  



Akizungumza katika hafla hiyo, Herry James aliwashukuru waandaaji na washiriki wa mafunzo haya kwa kujitokeza kwa wingi, akisisitiza umuhimu wa mafunzo haya katika kuongeza uelewa wa masuala ya demokrasia, haki za binadamu, utawala bora, na majukumu ya vyombo vya ulinzi na usalama.  

Mratibu wa Mafunzo hayo Bi Dorice Dario,Wakili Mkuu daraja la kwanza (principal state Attorney) kutoka idara ya Katiba na ufuatiliaji haki Wizara ya katiba na sheria.


“Lengo kuu la mafunzo haya ni kuwajengea uwezo viongozi katika ngazi mbalimbali za utawala ili kuhakikisha tunazingatia misingi ya utawala bora, haki za binadamu, na demokrasia kwa vitendo,” alisema.  

Kiongozi huyo alibainisha kuwa mafunzo haya yanahusisha wajumbe wa Kamati za Usalama za Mkoa na Wilaya, baadhi ya wataalam wa Halmashauri, na Watendaji wa Kata zote za Mkoa wa Iringa. Pia alieleza kuwa mafunzo ya ngazi ya Halmashauri yatafanyika kwa Kamati za Usalama za Wilaya, wataalam, na watendaji wa kata.  

Changamoto Zinazokabili Mkoa wa Iringa

Katika hotuba yake, Herry James alieleza changamoto mbalimbali zinazokabili Mkoa wa Iringa, zikiwemo uelewa mdogo wa haki za binadamu, mila na desturi kandamizi, vitendo vya ukatili wa kijinsia, pamoja na imani za kishirikina. Alitoa wito kwa washiriki wa mafunzo hayo kushirikiana kutatua changamoto hizi kwa kushirikisha maarifa watakayopata.  

Msaada wa Kisheria wa Mama Samia 

Akigusia kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia (Mama Samia Legal Aid Campaign), alisema kuwa kampeni hiyo imekuwa msaada mkubwa kwa wananchi katika mikoa mbalimbali. Alitoa wito kwa viongozi na watendaji wa Mkoa wa Iringa kushiriki kikamilifu kuhamasisha wananchi kutumia huduma za msaada wa kisheria zinazotolewa bure kupitia kampeni hiyo.  

Akihitimisha hotuba yake, Herry James aliwahimiza washiriki kuhakikisha kuwa maarifa yatakayotolewa yanakuwa chachu ya mabadiliko katika utendaji wao wa kila siku. “Ni wajibu wetu kuhakikisha kuwa elimu hii inasambazwa kuanzia ngazi ya familia hadi sehemu za kazi ili kujenga jamii yenye haki, amani, na utawala bora,” alisisitiza.  

Aliwatakia washiriki mafunzo yenye tija na mafanikio, huku akitoa pongezi kwa Wizara ya Katiba na Sheria pamoja na wawezeshaji wote kwa kufanikisha mafunzo haya.  

Mafunzo haya sasa yamefunguliwa rasmi na yanatarajiwa kutoa mwelekeo mpya katika usimamizi wa haki za binadamu, utawala bora, na demokrasia ndani ya Mkoa wa Iringa.  

Mungu Ibariki Tanzania! 


 

Jumanne, 10 Desemba 2024

KIWANDA CHA SUKARI MKULAZI, NGUZO YA MAENDELEO YA KILIMO NA VIWANDA TANZANIA

 

Kiwanda cha Sukari Mkulazi ni mojawapo ya miradi mikubwa ya maendeleo ya viwanda nchini Tanzania, kilichobuniwa kwa lengo la kukuza sekta ya kilimo, kupunguza utegemezi wa sukari ya nje, na kuimarisha uchumi wa ndani. Kiwanda hiki kipo katika Wilaya ya Morogoro Vijijini, mkoa wa Morogoro, na kimekuwa mfano wa mafanikio ya juhudi za serikali katika kufanikisha uchumi wa viwanda.

 

Historia na Maendeleo

Kiwanda cha Sukari Mkulazi kilianzishwa chini ya usimamizi wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) na Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF). Mradi huu ulianza rasmi mwaka 2018 na ulitengenezwa ili kushughulikia mahitaji ya sukari ambayo yamekuwa yakiongezeka kwa kasi nchini Tanzania.

 


Uwekezaji na Uwezo wa Uzalishaji

Kiwanda cha Mkulazi ni moja ya viwanda vikubwa vya sukari barani Afrika. Uwekezaji wake unakadiriwa kufikia zaidi ya TZS bilioni 500. Kina uwezo wa kuzalisha zaidi ya tani 200,000 za sukari kwa mwaka, kiwango ambacho kinachangia kwa kiasi kikubwa kupunguza nakisi ya sukari nchini. 

 

Ajira na Faida kwa Jamii

Mradi wa Mkulazi umetoa maelfu ya ajira kwa wakazi wa maeneo ya jirani na kwa taifa kwa ujumla. Wakulima wa miwa, ambao ni sehemu ya mnyororo wa thamani wa kiwanda, wamepata fursa ya kuuza mazao yao moja kwa moja kwa kiwanda kwa bei yenye ushindani. Pia, kiwanda kimechangia katika kuboresha miundombinu kama barabara, huduma za afya, na elimu katika maeneo ya karibu.

 


Changamoto na Mafanikio

Kama ilivyo kwa miradi mingi mikubwa, Mkulazi imekumbana na changamoto kama upatikanaji wa mitaji ya ziada, ukosefu wa teknolojia ya kisasa kwa baadhi ya nyanja, na masuala ya mazingira yanayohusiana na kilimo cha miwa. Hata hivyo, juhudi za serikali na sekta binafsi zimeendelea kuboresha hali hiyo.

 

Mchango kwa Uchumi wa Tanzania

Kiwanda cha Sukari Mkulazi kinachangia pakubwa katika kufanikisha malengo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano (FYDP III) unaolenga kukuza sekta ya viwanda. Kiwanda hiki kimepunguza kwa kiasi kikubwa gharama za uagizaji wa sukari kutoka nje, hivyo kuokoa fedha za kigeni na kuongeza mapato ya ndani.

 


Mustakabali wa Mkulazi

Katika miaka ijayo, Mkulazi inatarajia kupanua shughuli zake kwa kuongeza mashamba ya miwa, teknolojia za kisasa, na kuimarisha ushirikiano na wakulima wa maeneo mbalimbali. Hii itasaidia kufanikisha malengo ya kujitosheleza kwa sukari na kuchangia katika maendeleo endelevu ya kijamii na kiuchumi.

 

Kiwanda cha Sukari Mkulazi kinabakia kuwa alama ya ushindi wa Tanzania katika kuimarisha sekta ya viwanda na kilimo, ikiakisi dira ya maendeleo ya uchumi wa kati ifikapo 2025.


Jumamosi, 7 Desemba 2024

TANZANIA YAENDELEA KUNG'ARA KATIKA SEKTA YA USAFIRI WA ANGA, ONGEZEKO LA ABIRIA, USALAMA WA JUU, NA UWEKEZAJI WA MIUNDOMBINU

 

Sekta ya usafiri wa anga nchini Tanzania imeonyesha maendeleo makubwa katika miaka ya hivi karibuni, ikichangia kwa kiasi kikubwa katika ukuaji wa uchumi na kuimarisha nafasi ya nchi katika usafiri wa anga barani Afrika.

 

Ongezeko la Idadi ya Abiria na Mizigo

Katika kipindi cha miaka 20 iliyopita, idadi ya abiria wanaosafiri kwa njia ya anga imeongezeka kwa zaidi ya mara mbili, kutoka abiria 1,662,452 mwaka 2003 hadi abiria 4,614,380 mwaka 2023. Vilevile, usafirishaji wa mizigo umeongezeka kutoka tani 33,255 mwaka 2003 hadi tani 55,806.20 mwaka 2023. 


Kuboresha Usalama wa Anga

Katika ukaguzi uliofanywa na Shirika la Usafiri wa Anga Duniani (ICAO) mwezi Mei 2023, Tanzania ilipata alama 86.7, ikiifanya kushika nafasi ya nne barani Afrika katika masuala ya usalama wa anga, ikitanguliwa na Nigeria, Kenya, na Ivory Coast. 

 

Mchango katika Pato la Taifa

Sekta ya uchukuzi, ikijumuisha usafiri wa anga, ilichangia asilimia 8.2 ya Pato la Taifa kwa mwaka 2022, ikiashiria umuhimu wake katika uchumi wa nchi. 

 


Uwekezaji katika Miundombinu

Serikali imewekeza katika kuboresha viwanja vya ndege na kuongeza idadi ya ndege, hatua ambazo zimeimarisha huduma za usafiri wa anga na kuvutia wawekezaji na watalii zaidi nchini.

 

Maendeleo haya yameiwezesha Tanzania kuwa miongoni mwa nchi zinazoongoza katika usafiri wa anga barani Afrika, ikichangia katika ukuaji wa sekta nyingine kama utalii na biashara.

TANZANIA YAPAA KATIKA UZALISHAJI WA ASALI, NAFASI YA PILI BARANI AFRIKA NA FURSA MPYA SOKONI



Tanzania inazalisha wastani wa tani 33,276 za asali na tani 1,913 za nta kwa mwaka. Hata hivyo, kiwango hiki ni chini ya uwezo wa uzalishaji unaokadiriwa kufikia tani 138,000 za asali kwa mwaka. 

 

Katika soko la kimataifa, Tanzania inashika nafasi ya pili barani Afrika kwa uzalishaji wa asali, ikitanguliwa na Ethiopia.  Hata hivyo, ni asilimia tano tu ya asali inayozalishwa nchini ndiyo inauzwa nje ya nchi, huku asilimia 95 ikibaki katika masoko ya ndani. 

 

Mnamo Agosti 2024, Tanzania ilisaini makubaliano na China kuruhusu uuzaji wa asali katika soko la China, ambalo lina mahitaji ya tani milioni 38 kwa mwaka. Hii ni fursa muhimu kwa wafugaji nyuki na wafanyabiashara wa asali nchini kuongeza uzalishaji na kuuza katika soko hilo kubwa. 

 

Ili kuhakikisha ubora wa asali inayouzwa nje, serikali imezindua nembo ya asali ya Tanzania itakayotumika kuitambulisha bidhaa hiyo katika soko la dunia. Nembo hii inawahakikishia walaji kuwa bidhaa wanayotumia iko salama na inakidhi viwango vya ubora. 

 

Pamoja na jitihada hizi, bado kuna changamoto katika kuongeza uzalishaji na mauzo ya asali nje ya nchi. Serikali inaendelea kuweka mazingira wezeshi kwa wafugaji nyuki kwa kutenga maeneo maalum ya kufugia nyuki na kujenga viwanda vya kuchakata na kufungasha mazao ya nyuki katika mikoa mbalimbali. 

 

Kwa ujumla, Tanzania ina nafasi nzuri katika uzalishaji wa asali barani Afrika na inaendelea kuchukua hatua za kuboresha uzalishaji na kuongeza ushiriki wake katika soko la kimataifa.

VIJANA WAVUNA DHAHABU YA SAMAKI ZIWA VICTORIA: UWEKEZAJI WA VIZIMBA NA UMEME WA JUA CHINI YA UFADHIRI WA TADB WAFUNGUA MILANGO YA AJIRA NA UTAJIRI MPYA TANZANIA

Ufugaji wa samaki kwa kutumia vizimba ndani ya Ziwa Victoria umeanza kuwa nguzo muhimu ya kuimarisha uchumi wa vijana na kuchangia usalama w...