Alhamisi, 12 Desemba 2024

OFISI YA MKUU WA WILAYA NJENDENGWA, DODOMA: ALAMA YA MAENDELEO CHINI YA UONGOZI WA MHE. DKT. SAMIA SULUHU HASSAN

Dodoma, Tanzania - Ofisi ya Mkuu wa Wilaya iliyopo Njendengwa, ndani ya Jiji la Dodoma, ni mojawapo ya miradi muhimu ya ujenzi iliyotekelezwa katika awamu ya sita ya uongozi chini ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan. 

Jengo hili limejengwa kwa kuzingatia viwango vya kisasa, likiwa na miundombinu ya kisasa inayolenga kuboresha utoaji wa huduma za utawala na maendeleo kwa wananchi wa Wilaya hiyo. Kukamilika kwa jengo hili ni sehemu ya jitihada za serikali kuhakikisha miundombinu ya kisiasa na kiutawala inaimarishwa, ikiwa ni ishara ya dhamira ya Rais Samia katika kuleta maendeleo yenye tija kwa Taifa.  

Aidha, ujenzi wa ofisi hii ni sehemu ya mpango mpana wa serikali ya awamu ya sita wa kuboresha huduma kwa wananchi kwa kuhakikisha watendaji wa serikali wanakuwa na mazingira bora ya kufanyia kazi, hatua inayochangia ufanisi wa utoaji huduma na maendeleo katika ngazi za wilaya na mikoa.  

Wananchi wa Dodoma wamesifu juhudi za serikali kwa kuona kuwa Wilaya ya Dodoma imepewa kipaumbele, huku wakibainisha kuwa jengo hili litachochea maendeleo ya kiutawala na kijamii katika eneo hilo.  

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

VIJANA WAVUNA DHAHABU YA SAMAKI ZIWA VICTORIA: UWEKEZAJI WA VIZIMBA NA UMEME WA JUA CHINI YA UFADHIRI WA TADB WAFUNGUA MILANGO YA AJIRA NA UTAJIRI MPYA TANZANIA

Ufugaji wa samaki kwa kutumia vizimba ndani ya Ziwa Victoria umeanza kuwa nguzo muhimu ya kuimarisha uchumi wa vijana na kuchangia usalama w...