Jumanne, 28 Oktoba 2025

RIPOTI YA HALI YA UCHAGUZI MKUU – TANZANIA

Tarehe: 29 Oktoba 2025

Muda: Asubuhi (kuanzia saa 12:30 alfajiri – 02:10 asubuhi)
Chanzo: Taarifa za moja kwa moja kutoka kwa wananchi walioko vituoni maeneo mbalimbali nchini.

Muhtasari wa Jumla wa Hali ya Uchaguzi

Asubuhi ya leo Watanzania wamejitokeza kwa wingi katika vituo vya kupigia kura nchi nzima. Hali ya jumla imeendelea kuwa shwari, yenye amani, usalama na utulivu.
Vituo vingi vimefunguliwa kwa wakati, maandalizi yamekamilika na wapiga kura wanafuata taratibu kwa utulivu.

Mwitikio mkubwa umeonekana takribani mikoa yote iliyoripotiwa, na raia wengi wakisisitiza umuhimu wa kutimiza haki ya msingi ya kikatiba kupiga kura.

Ripoti kwa Mujibu wa Mikoa na Maeneo

✅ Dodoma

  • Bahi – Mwitikio mzuri wa wananchi; hali ni shwari.

  • Kongwa – Uhamasishaji mkubwa, wananchi wanaendelea kupiga kura kwa amani.

Mazingira: Rafiki, ulinzi umeimarishwa, utaratibu unazingatiwa.


✅ Simiyu

  • Bariadi Mji – Kituo cha Majengo

    • Kimefunguliwa mapema

    • Majina yamebandikwa vizuri

    • Makarani wanatoa maelekezo

    • Zoezi lilianza saa moja kamili asubuhi



✅ Kilimanjaro

  • Same – Wapiga kura wamejitokeza mapema, usalama na hamasa kubwa kuripotiwa.



✅ Kagera

  • Karagwe – Mvua ndogo inakumba eneo lakini bado wananchi wanaendelea na zoezi bila kusita.



✅ Lindi

  • Lindi Manispaa

    • Shughuli za kupiga kura zinaendelea sambamba na shughuli za uchumi

    • Biashara zimefunguliwa na usafiri unaendelea kama kawaida

  • Ruangwa – Malolo

    • Zozi linaendelea vizuri tangu mapema

  • Mtama – Nang’aka

    • Wapiga kura wanatiki na kurejea nyumbani kwa utulivu


✅ Rukwa

  • Nkasi – Nkomolo
    Zoezi linaendelea kwa amani.

  • Sumbawanga – Mtaa wa Chemka 1
    Foleni inaendelea, uhamasishaji ni mzuri.

    Wananchi wakiendelea kupiga kura katika kituo cha MTAA WA CHEMKA-1 kilichopo mtaa wa Chemka Kata ya Msua Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga Mkoani Rukwa.

    Utulivu wa kutosha kijiji cha Isunta, kata ya isunta halmashauri ya wilaya ya nkasi, mkoa wa Rukwa.


✅ Njombe

  • Makambako – Kivavi
    Hali ya utulivu, wananchi wapo vituoni mapema.


✅ Mtwara

  • Masasi Mjini – Migongo, Nangaya A
    Zoezi linaenda kwa utaratibu mzuri; wananchi wanatimiza haki kisha kurejea kwenye shughuli zao.




✅ Mwanza

  • Nyamagana – Nyamanoro, Kituo cha Nkubi
    Mwitikio upo lakini changamoto ndogo:

    • Baadhi ya makarani hawatoi msaada wa kutosha kwa wapiga kura.
      (Taarifa imetolewa kwa mujibu wa mwakilishi)


✅ Kusini Unguja na maeneo mengine

— Hakuna changamoto kubwa zilizoripotiwa katika taarifa za asubuhi.


✅ AUSHA

Mtaa wa Korongoni, Kata ya Lemara, Wilaya ya Arusha Mjini wananchi wanaendelea na zoezi la kupiga kura ili hali vifaa vilichelewa kidogo. Kuna utulivu.


Wilaya ya Namtumbo,Kata ya Namtumbo,Mtaa wa Lusenti,Kituo cha Lusenti.



3️⃣ Uhamasishaji na Ushiriki wa Wananchi

Ujumbe mwingi wa hamasa umetolewa na wananchi, ukiwahimiza wengine kujitokeza mapema na kutimiza wajibu wao wa kikatiba:

“Siku niliyoisubiri na kuiombea kwa ham ni leo… Nimetimiza haki yangu ya msingi ya kikatiba kupiga kura.”

Hashtags zilizotumika sana:
#KidoleNaWino ✅ | #KidoleNaTiki ✅ | #NdioLeo


4️⃣ Usalama na Taratibu

  • Ulinzi umeimarishwa katika vituo vingi

  • Makarani wanaongoza utaratibu vizuri

  • Hakuna vurugu wala taharuki kuripotiwa asubuhi hii


5️⃣ Changamoto Zilizobainishwa

  • Huduma kwa wapiga kura: Mwanza (Nyamanoro) – usaidizi kwa baadhi ya wapiga kura si wa kuridhisha

  • Hali ya hewa: Karagwe – mvua ndogo lakini hakuna athari kubwa


6️⃣ Hitimisho la Awali

Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 umeanza kwa muitikio mkubwa, amani na utulivu. Wananchi wanaendelea kutimiza wajibu wao kwa nidhamu na uzalendo.

Ripoti hii itaendelea kusasishwa kadri taarifa mpya zinavyopokelewa kutoka vituo mbalimbali nchini.



Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Kagera River Girls: Uwekezaji wa Bilioni 4.1 Unaobadilisha Ndoto za Wasichana Kuwa Mafanikio ya Taifa

Katika Wilaya ya Karagwe, Kata ya Kanoni, kunasimama kwa fahari  Shule ya Sekondari Kagera River Girls —taa ya matumaini na ushahidi hai kwa...