MUHAS KUANZA MAFUNZO MAALUM KWA GYM INSTRUCTORS ILI KUBORESHA USALAMA WA MAZOEZI KWA WAGONJWA

 

CHUO Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) kinatarajia kuanza kutoa mafunzo maalum ya kitaalamu kwa wakufunzi wa mazoezi ya viungo (gym instructors) na wasimamizi wa kumbi za mazoezi (fitness managers),ili kuhakikisha wanakuwa na uwezo wa kuwahudumia wateja wanaopelekwa kufanya mazoezi kwa sababu za kitabibu.


Akizungumza leo Mei21,2025 wakati wa uzinduzi wa kambi ya siku mbili ya uchunguzi wa afya ya moyo bila malipo katika Kampasi ya MUHAS Mloganzila,Makamu Mkuu wa Chuo hicho, Profesa Appolinary Kamuhabwa moja amesema mpango huo unalenga kulinganisha huduma za mazoezi ya viungo ya viwango vya kitaifa vya afya.


“Uzoefu unaonesha kuwa watu wengi huanza mazoezi bila ushauri wa kitabibu, jambo ambalo linaweza kuwa hatari kwa afya hususani moyo,” amesema Profesa Kamuhabwa.


Ameongeza,“Lengo letu ni kuwajengea uwezo waendeshaji wa kumbi za mazoezi ili waweze kutoa huduma kwa kufuata taratibu za kitaalamu za afya,”


Ameonya suala la jamii kufanya mazoezi bila usimamizi wa kitabibu kunaweza kusababisha madhara makubwa, ikiwa ni pamoja na kupoteza maisha ghafla kwa watu wenye magonjwa ya moyo au matatizo mengine ya kiafya yaliyofichika.


Profesa Kamuhabwa amesema kama sehemu ya mpango huo, MUHAS itazindua kituo kipya cha mazoezi ya viungo mapema wiki hii, ambacho kitakuwa kinatoa vyeti vya mazoezi kama ilivyo kwa dawa zinazotolewa kwa agizo la daktari.


Amesema mafunzo hayo pamoja na uanzishaji wa gym hiyo ni sehemu ya jitihada za kuboresha kiwango cha huduma za mazoezi ya viungo nchini na kupunguza hatari za kiafya kutokana na mazoezi yasiyo na miongozo ya kitaalamu.


Akizungumzia kambi ya uchunguzi inayoendelea, Profesa Kamuhabwa amesema shughuli mbalimbali zinazofanyika kuelekea uzinduzi wa awamu ya pili ya Kituo cha Umahiri cha Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) ni pamoja na huduma za magonjwa ya moyo, kinga na tiba kwa wale watabainika kuwa na matatizo ya moyo.


Kwa upande wake, mtaalamu wa fiziolojia Irine Mngolokolo,amesema gym hiyo mpya imeundwa mahsusi kwa ajili ya watu wenye changamoto za kiafya.


Irene ambaye pia ni msaidizi wa kufundisha katika kituo hicho amesisitiza umuhimu wa kuanza mazoezi kwa mpango maalum uliopangwa na mtaalamu, iwe ni ya aerobic au anaerobic, kulingana na mahitaji ya mhusika.


Makamu Mkuu wa Chuo Taaluma, Profesa Emmanuel Balandya, amesema kuwa mafunzo ya wataalamu wa afya ya moyo ni moja ya vipaumbele vikuu vya MUHAS.

Comments

  1. Ni hatua muhimu katika kuboresha na kuimarisha afya

    ReplyDelete
  2. Yote hii ni juhudi za Serikali katika kuhakikisha afya ya Mtanzania inapewa kipaumbele hongera sana kwa Jemedari Mh Dkt Samia Suluhu Hassan 🔥

    ReplyDelete

Post a Comment

Popular posts from this blog

JE, KAULI MBIU YA MHE. RAIS, DKT. SAMIA SULUHU HASSAN – 'KAZI NA UTU TUNASONGA MBELE' INA MAANA GANI KWA MAENDELEO YA TANZANIA?

UMUHIMU WA ZIARA YA RAIS WA TFF KUKAGUA UJENZI WA UWANJA WA MPIRA WA MIGUU ARUSHA – KWA ULIMWENGU WA SOKA NA USTAWI WA TAIFA