UJENZI WA UWANJA WA MPIRA WA MIGUU KMC KIJITONYAMA MWENGE WAKAMILIKA NA KUANZA KUTUMIKA

Leo, timu ya wataalamu na viongozi kutoka Manispaa ya Kinondoni ilifanya ziara ya kutembelea na kukagua uwanja huo, ambapo waliridhishwa na kiwango cha ujenzi na maandalizi yaliyofanywa kuhakikisha uwanja huo unakuwa wa viwango vya kisasa.
Uwanja huu unatarajiwa kuwa chachu ya maendeleo ya michezo, hususan soka, kwa vijana wa Kinondoni na maeneo jirani, huku ukiwapa fursa ya kukuza vipaji na kushiriki mashindano mbalimbali.
Manispaa ya Kinondoni inaendelea kuwekeza katika sekta ya michezo kama sehemu ya juhudi za kukuza afya, kuimarisha mshikamano wa jamii, na kuandaa vipaji vitakavyoiwakilisha Tanzania katika ngazi za kitaifa na kimataifa.
Wananchi na wapenzi wa michezo wamehimizwa kuutumia uwanja huu ipasavyo ili kuhakikisha dhamira ya serikali ya kuimarisha michezo inatimia.
Kazi inaendelea, Tanzania 🇹🇿 yetu nzuri
ReplyDelete