Ijumaa, 14 Februari 2025

RAIS SAMIA AWASILI ADDIS ABABA KUSHIRIKI MKUTANO WA 38 WA WAKUU WA NCHI NA SERIKALI WA AU

 

Addis Ababa, Ethiopia – Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amewasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Bole, Addis Ababa, Ethiopia, leo Februari 14, 2025, kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Kawaida wa 38 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Umoja wa Afrika (AU).  

Katika mkutano huo, viongozi wa mataifa wanachama wa AU watajadili masuala mbalimbali yanayohusu maendeleo, usalama, na mustakabali wa bara la Afrika. Mbali na kuhudhuria mkutano huo wa kilele, Mhe. Rais Dkt. Samia pia atashiriki katika Mkutano wa Baraza la Amani na Usalama la Umoja wa Afrika, ambapo mijadala itahusu juhudi za kudumisha amani, utatuzi wa migogoro, na ushirikiano wa kikanda katika kuhakikisha ustawi wa Afrika.  


Safari hii ya Mhe. Rais inasisitiza dhamira ya Tanzania katika kushiriki kikamilifu katika mijadala ya kimataifa na kuendelea kuunga mkono ajenda za maendeleo, amani, na mshikamano wa bara la Afrika.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

VIJANA WAVUNA DHAHABU YA SAMAKI ZIWA VICTORIA: UWEKEZAJI WA VIZIMBA NA UMEME WA JUA CHINI YA UFADHIRI WA TADB WAFUNGUA MILANGO YA AJIRA NA UTAJIRI MPYA TANZANIA

Ufugaji wa samaki kwa kutumia vizimba ndani ya Ziwa Victoria umeanza kuwa nguzo muhimu ya kuimarisha uchumi wa vijana na kuchangia usalama w...