Jumanne, 25 Novemba 2025
Jumatatu, 24 Novemba 2025
Alhamisi, 20 Novemba 2025
Tanzania:ukurasa mpya wa amani kwa kuzindua Tume Huru ya Uchunguzi wa Matukio ya Uvunjifu wa Amani
Dodoma, 20 Novemba 2025 — Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, alizindua rasmi Tume Huru ya Uchunguzi wa Matukio ya Uvunjifu wa Amani yaliyotokea wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu uliofanyika tarehe 29 Oktoba, 2025, katika hafla iliyofanyika Ikulu Chamwino, Dodoma. Tukio hilo lilikuwa na lengo la kuimarisha misingi ya demokrasia na utulivu wa nchi kwa njia ya uchunguzi wa kina, haki na uwazi.
Jumatatu, 17 Novemba 2025
Jumamosi, 15 Novemba 2025
Alhamisi, 6 Novemba 2025
Kilwa Kisiwani Yazidi Kutesa: Watalii 147 Wavutiwa na Urithi wa Kihistoria wa Tanzania
Hifadhi ya Urithi wa Dunia ya Kilwa Kisiwani na Songo Mnara imeendelea kuthibitisha upekee wake kwenye ramani ya utalii duniani. Tarehe 31 Oktoba 2025, msimu wa utalii ulipamba moto baada ya meli ya kifahari SH Diana kutia nanga na kuleta wageni 147 kutoka mataifa 13 tofauti.
Ufaransa, Australia, Ubelgiji, Canada, Uingereza, Uswisi, Ujerumani, Cyprus, New Zealand, Marekani, Urusi, Uturuki na Ukraine — zote zilikuwa na mguu mmoja Kilwa. Wageni hawa walihamasishwa na uhondo wa historia na urithi wa usanifu wa mawe uliotamba katika karne za kati, eneo ambalo UNESCO imelipa hadhi ya Urithi wa Dunia tangu 1981.
Historia Inayotembea: Wageni Wajionea Alama za Usultani
Wakiwa chini ya uratibu wa Savannah Tours Ltd kwa kushirikiana na Black Willow Safaris, watalii hao walipata nafasi ya kutembea maeneo nyeti ya kihistoria kama vile:
Msikiti Mkongwe uliojengwa kwa mawe ya matumbawe
Kasri la Sultani — kiini cha nguvu za biashara ya kimataifa
Maeneo kadhaa yaliyokuwa kitovu cha biashara ya dhahabu, pembe za ndovu na bidhaa kutoka bara na ng’ambo
Wataalamu wa malikale kutoka TAWA waliwapa wageni hao simulizi zinazofufua uhalisia wa maisha ya kale — simulizi zinazong’ara zaidi kuliko mawe ya majengo yenyewe.
Kauli ya Uongozi wa Hifadhi
Kamanda wa Hifadhi, Kelvin Stanslaus, alisema ujio wa wageni hao unaibua matumaini mapya kwa ukuaji wa utalii wa urithi:
“Tunayo furaha kubwa kuona wageni kutoka pande mbalimbali za dunia wakija kujionea historia adhimu ya Kilwa, ambayo ni alama muhimu ya biashara ya kimataifa ya karne za kati kati ya Afrika Mashariki na Dunia.”
Kwa mujibu wa Stanslaus, safari kama hizi zinatoa taswira ya namna Tanzania inavyozidi kuvutia soko la utalii la kimataifa — si kwa vivutio vya wanyamapori pekee, bali pia urithi wa kitamaduni.
Utalii wa Urithi Wazidi Kushika Hatamu
TAWA ilisema kuwa ongezeko la safari za meli kubwa kama SH Diana ni matokeo ya mkakati mpana wa Serikali kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii katika kukuza utalii wa:
Bahari
Maeneo ya malikale
Visiwa vyenye thamani kuu ya kihistoria
Uwekezaji huu unachochea ajira kwa jamii zinazozunguka hifadhi, kukuza biashara ndogondogo na kutangaza utamaduni wa Kitanzania kwa upekee wa kimataifa.
Kilwa: Dhahabu Iliyofichwa Baharini
Kwa miongo kadhaa, Kilwa Kisiwani imebaki kuwa hazina iliyosubiri kusimuliwa zaidi, na sasa dunia inaendelea kugeuza macho yake hapa. Wageni wanaondoka wakiwa na kumbukumbu zinazotengenezwa na historia, maji ya bluu ya bahari na ukarimu wa watu wa Kilwa.
Na kama ilivyo kwa kila anayefika, swali hubaki:
Ni lini utakuja kujionea mwenyewe?
Jumatatu, 3 Novemba 2025
TATHMINI YA KITAALAMU KUHUSU SHEREHE ZA UAPISHO WA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
-
Kauli mbiu ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan –"Kazi na Utu Tunasonga Mbele" – ni dira ya maende...
-
1. Utangulizi Mjadala huu umeibua fikra pevu, zenye msukumo wa kiroho, kijamii, na kiuchumi kuhusu nafasi ya fikra, matendo, na amani kat...
-
1. Mtazamo wa Kijumla: Maliasili kama Hazina ya Taifa Mjadala huu umeonyesha kwa uwazi kwamba Watanzania wengi wanatambua maliasili kama u...
.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)


.jpeg)



.jpeg)









.jpeg)



.jpeg)
.jpeg)


.jpeg)



