Tanzania Bila Plastiki Inawezekana! Tuchukue Hatua Leo kwa Mazingira Bora Kesho SIKU YA MAINGIRA DUNIANI "Mazingira Yetu na Tanzania Ijayo: Tuwajibike Sasa, Dhibiti Matumizi ya Plastiki" ni ujumbe mzito na wa kina unaoangazia wajibu wa kizazi cha sasa katika kulinda mazingira kwa ajili ya ustawi wa taifa la baadaye. 1. "Mazingira Yetu" — Tunacholinda Leo Maneno haya yanatambua kuwa mazingira ni rasilimali ya wote – ardhi, mito, misitu, bahari, hewa na viumbe hai. Kauli hii inahimiza watu wote kutambua kwamba: Mazingira ni msingi wa maisha yetu ya kila siku , yakiwemo afya, kilimo, nishati, utalii na hata utamaduni wetu. Mazingira yetu yameanza kuathirika kwa kasi kutokana na uharibifu unaochangiwa na binadamu – ukataji miti ovyo, utupaji taka hovyo, uchafuzi wa maji na hewa, na zaidi sana, matumizi mabaya ya plastiki. 2. "Na Tanzania Ijayo" — Hatima ya Taifa Ipo Mikononi Mwetu Hili ni wito wa kuangalia mbali. Kauli hii inaonyesha kuwa: Mustakabali ...