Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania leo, Februari 12, 2025, jijini Dodoma, limepitisha Muswada wa Marekebisho ya Sheria ya Usimamizi wa Mazingira wa Mwaka 2024 baada ya kufanyiwa marekebisho kutoka katika mapendekezo ya Serikali.
Akiwasilisha maelezo ya muswada huo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhe. Hamad Yusuf Masauni, alisema marekebisho hayo yanalenga kuendana na Sera ya Taifa ya Mazingira ya 2021 na kutatua changamoto za utekelezaji wake.
Marekebisho muhimu yaliyofanywa ni pamoja na:
- Kumpa Waziri mamlaka ya kusimamia na kudhibiti masuala ya mabadiliko ya tabianchi.
- Kuanzisha Kituo cha Taifa cha Kuratibu Kaboni (NCMC) ili kurasimisha shughuli zake na kuwezesha ushiriki katika mikataba ya kitaifa na kimataifa kuhusu biashara ya kaboni.
- Kuongeza vitengo vya usimamizi wa mazingira katika wizara na taasisi mbalimbali ili kushughulikia masuala ya mabadiliko ya tabianchi.
- Kuimarisha mfumo wa kitaasisi kwa kuibadilisha Kamati ya Taifa ya Ushauri wa Mazingira kuwa Kamati ya Taifa ya Mabadiliko ya Tabianchi.
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Maji na Mazingira, kupitia Mhe. Agnes Hokororo, imepongeza marekebisho hayo na kushauri kuanzishwa kwa sheria mpya zitakazofanya Baraza la Taifa la Mazingira kuwa mamlaka kamili pamoja na sheria kuhusu uchumi wa buluu.
Baada ya kupitishwa na Bunge, muswada huo sasa utawasilishwa kwa Rais kwa ajili ya kusainiwa na kuwa sheria kamili.
Kazi iendelee, nchi ipo swari na watu tunaendelea na shughuli za uzalishaji kama kawaida🇹🇿
JibuFuta#MSLAC #Katibanasheria #SSH #CCM #KaziIendelee #Nchiyangukwanza #SisiniTanzania #matokeochanya