Jumatano, 4 Desemba 2024

 UONGOZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA INAYOHUSIKA NA HAKI ZA BINADAMU NA WATU YAKUTANA NA UONGOZI WA WIZARA YA KATIBA NASHERIA



Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Prof Palamagamba John Kabudi leo tarehe 04 Desemba, 2024 amekutana na kufanya kikao na  Rais wa Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu Mhe. Jaji Imani Aboud aliyeambatana  na ujumbe  kutoka Mahakama hiyo iliyopo jijini Arusha. 

Katika mazungumzo  hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa Wizara Mtumba, jijini Dodoma viongozi hao wamejadili kuhusu nafasi ya Mahakama  ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu katika kusimamia na kulinda Haki za Binadamu na Watu wa Afrika. 

Waziri Kabudi amesema yapo maeneo ambayo yanahitaji kuboreshwa zaidi katika Mahakama ili kuimarisha mahusiano mazuri yaliyopo ambapo pia wamejadili changamoto zinazoikabili sekta ya Mahakama ambapo wamekubaliana kuendeleza majadiliano kwa ajili ya kuzifanyia kazi changamoto hizo ili kuiwezesha Mahakama kutimiza majukumu yake ambayo imepewa chini ya Mkataba wa kuanzishwa kwa  Mahakama hiyo. 





Rais wa Mahakama ya Afrika ya haki za binadamu na wału Mhe. Jaji Imani Aboud akiteta jambo na Katibu Mkuu wizara ya katiba na sheria Bwana Eliakimu Maswi akiambatana na Naibu Katibu Mkuu Dkt.Franklin Rwezimula





Sambamba na hilo maeneo mengi ya majadiliano ni pamoja na kuimarisha ushirikiano katika eneo la Rasilimali Watu ili kuwajengea uwezo Maafisa wa Mahakama kwa kupata mafunzo na uzoefu katika Mahakama hiyo ili Tanzania iweze kutoa mchango wake katika utekelezaji wa kazi za Mahakama hiyo. 

Viongozi hao pia wamepitia mambo ambayo Tanzania inawajibu wa kuyatekeleza chini ya Mkataba wa kuwa  Mwenyeji wa Mahakama hiyo. 




Katika hatua nyingine Waziri Kabudi Kabudi amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuridhia kutoa fedha  kwa ajili ya ujenzi wa jengo kubwa la Mahakama Afrika, ambapo amesema kuwa mambo mengi yanayofanywa katika Mahakama hiyo yanaendana na utekelezaji wa falsafa ya 4R ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ambayo ni  Maridhiano, Ustahimilivu, Kuboresha na Kujenga upya. 

Waziri Kabudi amesema kuwa kwa sasa  Wizara inaandaa Muswada wa utekelezaji wa mapendekezo ya Tume ya Haki Jinai na katika kufanya hivyo miongoni mwa nyaraka zitakazotumika ni pamoja na maamuzi ya Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu.

Maoni 3 :

  1. Vyombo vinavyoshughurikia masuala ya haki na Usawa vikifanya kazi Kwa pamoja kuboresha namna ya Utoaji huduma na hujenga Imani Kwa Wananchi katika haki na Usawa mbele ya Sheria.

    JibuFuta
  2. Kwa kutambuliwa katika katiba yetu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Haki za binadam,Basi kama Nchi tunapaswa kuzingatia sana hilo..Ni matumaini yetu kua tutaendelea kuheshimu ma kutambua haki za binadam kama ilivyo ainishwa katika katiba yetu.
    #SisiNiTanzania #SSH #Tanzania #MSLAC #Katibanasheria

    JibuFuta
  3. Tanzania imara 🇹🇿
    #SisiNiTanzania
    #matokeochanya
    #SSH

    JibuFuta

VIJANA WAVUNA DHAHABU YA SAMAKI ZIWA VICTORIA: UWEKEZAJI WA VIZIMBA NA UMEME WA JUA CHINI YA UFADHIRI WA TADB WAFUNGUA MILANGO YA AJIRA NA UTAJIRI MPYA TANZANIA

Ufugaji wa samaki kwa kutumia vizimba ndani ya Ziwa Victoria umeanza kuwa nguzo muhimu ya kuimarisha uchumi wa vijana na kuchangia usalama w...