Baadhi ya wananchi waliohudhuria fainali ya mpira wa miguu iliyofanyika katika viwanja vya Chuo Kikuu cha Mtakatifu John, jijini Dodoma, wamepongeza jitihada zinazofanywa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kupitia Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA), kwa kuendelea kuwekeza katika kinga na tiba ya waathirika wa dawa za kulevya pamoja na utoaji wa elimu endelevu kwa vijana. Michuano hiyo ya mpira wa miguu, ambayo imeandaliwa na Mamlaka ya kudhibiti na kupambana na dawa za kulevya DCEA, imekuwa sehemu ya jukwaa la kijamii kuhamasisha mapambano dhidi ya matumizi ya dawa za kulevya miongoni mwa vijana. Katika mchezo wa fainali uliovutia mamia ya mashabiki, timu ya Wagoloko FC iliibuka mshindi kwa kuifunga timu ya Mwaise FC mabao 2–0. Akizungumza wakati wa fainali hiyo, Mwalukasi Sidi Jonjolo, mmoja wa wananchi waliokuwepo uwanjani, alitoa wito kwa serikali kuhakikisha elimu kuhusu madhara ya dawa za kulevya inasambazwa zaidi ka...